
Msomaji wetu mmoja ametuandikia akitaka kujua alipo mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya,Besta(pichani) kwani hajamsikia kwa muda mrefu.Ukweli ni kwamba hata sisi hatuna jibu la uhakika ingawa fununu tulizonazo ni kwamba Besta alirejea nchini Uganda kumalizia masomo yake aliyokuwa ameyakatisha.Alikuwa anasomea masuala ya Habari na Tekinolojia.Besta aliwahi kutamba sana na wimbo wake Kati Yetu ambao unaweza kuutizama kwenye video hapo chini.Kama kuna mtu ambaye ana habari za uhakika zaidi,tusaidiane tafadhali.
No comments:
Post a Comment