
Hatimaye shindano hili la kumtafuta mrembo mwenye mvuto wa kimapenzi ‘Ijumaa Sexiest Girl’ limeingia kunako hatua ya fainali baada ya mshiriki wa kumi na saba, Neema Chande kutolewa leo.Neema ambaye ameambulia kura chache za kumtaka aendelee kuwepo katika shindano hili kutoka kwa wasomaji ambao ndiyo Majaji, ameuacha mpambano ukiendelea na warembo Irene Uwoya, Hadija Sure, Jokate Mwegelo, Wema Sepetu na Rose Ndauka ambao kwa pamoja wanakamilisha Top 5 hiyo.Kauli kutoka kwa mratibu wa mpambano huo, Oscar, kinachofuata hivi sasa ni kuzitafuta zile chati tatu za juu, yaani Top 3 kabla ya kumpata mshindi mmoja. Amewaomba wasomaji na wapenzi wa shindano hili waendelee kutuma kura zao kwa kuandika ujumbe mfupi wakimtaja mshiriki ambaye anastahili kuibuka na ushindi, kisha watume kwenda simu namba 0784-275 714.“Tunawashukuru na kuwapongeza washiriki wote waliyotolewa katika shindano hili, bila kuwasahau nyinyi wasomaji na wapenzi wa mpambano huu kwa kupiga kura zenu. Tunawaomba muendelee kuchangia mpaka pale mshindi mmoja, yaani ‘Ijumaa Sexioest Girl’ atakapopatikana,” alisema Oscar
No comments:
Post a Comment